Burudani
Designer Makeke apata dili jingine la ‘Rwanda Cultural Fashion Show’
Designer Makeke apata dili jingine la mitindo nchini Rwanda baada ya kufanya vizuri kwenye tamasha la East Africa Fashion Week lililofanyika nchini Kenya mwezi uliopita.
Joctan Makeke maarufu kama Makeke ambaye ni mmoja kati ya madesigner wanaofanya vizuri kwenye mitindo kwa sasa na ameiwakilisha vizuri Tanzania Kimataifa kwenye mitindo, amefanikiwa kupata mualiko mwingine nchini Rwanda kwenye tamasha la ‘Rwanda Cultural Fashion Show’.
Tamasha hilo lililoandaliwa na World Economic Fund na Benki kuu ya Rwanda litafanyika Mei 13 mwaka huu kwenye ukumbi wa Goethe Institute.
Hongera sana brother Makeke, mafanikio yako ni maendeleo kwa taifa la Tanzania.