Burudani

Mo Music kuachia wimbo mpya ‘Nitazoea’ Jumatatu Ijayo

Baada ya ukimya wa muda mrefu hit maker wa ‘Basi Nenda’ Moshi “Mo-Music” Katemi anatarajia kuachia wimbo wake mpya alioupa jina la ‘Nitazoea’.

MO nitazoea

Wimbo huo ambao utakuwa ni single ya nne kwa msanii huyo kutoka jiji la miamba Mwanza utatoka Jumatatu April 13.

‘Nitazoea’ ni wimbo wa Mapenzi ambao umetayarishwa na ma-producer watatu ambao ni Aby Daddy, Lollipop na D-Classic.

Uongozi wa Mo Music umeiambia Bongo5 kuwa video ya ‘Nitazoea’ itaanza kufanywa wiki ijayo na Adam Juma wa Next Level.

Nyimbo za Mo Music zilizopita kabla ya huu ni ‘Basi Nenda’ ambayo ilifanya vizuri kila kona ya nchi, na kufuatiwa na ‘Simama’ pamoja na Almasi ambazo zilitoka kwa pamoja mwishoni mwa mwaka jana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents