Tragedy
Mrembo wa Ufaransa aliyeigiza filamu kuhusu utekwaji, auawa kwenye shambulio la Westgate
Mrembo wa London raia wa Ufaransa, aliyewahi kuigiza kwenye filamu iliyohusu masuala ya kutekwa alikuwa mmoja wa watu waliouawa na magaidi kwenye shambulio la jengo la Westgate.
Anne Dechauffour, 27, na mama yake Corinne, 54, waliuawa wakiwa ndani ya gari na washambuliaji hao. Kwa mujibu wa ripoti, Anne alikuwa ameenda kumsalimia mama yake, msanii aliyekuwa ameolewa na kuhamia Kenya miaka 10 iliyopita.
Baba yake, Michel, anaaminika kumiliki hoteli ya kifahari ya Rock Leopard Lodge, kwenye hifadhi ya taifa ya Meru.