Picha
Mwanafunzi bora kidato cha sita 2015/16 akabidhiwa tuzo yake ya ASSA2016
Mwanafunzi aliyeongoza katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2015/16 nchini, Ramadhan N.Gembe wiki hii alikabidhiwa rasmi cheti chake cha tuzo za wanafunzi bora AfriKa Mashariki, ASSA 2016.
Gembe amekabidhiwa cheti chake wiki hii kutokana na kukosekana wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo hizo zilizofanyika July 29 mwaka huu kufuatia kubanwa na masomo.
Aaron ambaye ni mmoja wa waasisi wa tuzo hizo amesema kwa sasa wanandaa msimu wa pili wa ASSA, ikiwa ni pamoja na kuanzisha kipindi cha TV chenye lengo la kuleta hamasa ya masomo kwa njia ya elimu na burudani (edutainment) kwa vijana wa Afrika ambao bado wako mashuleni.
“Kipindi hiki ni sehemu ya kazi za kuelekea tuzo za wanafunzi bora, ambazo kilele chake ni mwezi Juni mwakani 2017,” amesema.