Michezo
Oscar Pistorius kutoka jela Jumanne ijayo
Mwanariadha mlemavu wa nchini Afrika Kusini, Oscar Pistorius ataachiwa kutoka gerezani Jumanne ijayo baada ya bodi ya parole kutoa ruhusa.
Pistorius alihukumiwa kwenda jela miaka mitano kwa kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp mwaka 2013. Amekaa jela kwa mwaka mmoja sasa.
Hata hivyo bado anakabiliwa na rufaa kwenye mahakama kuu mwezi ujao ambayo kama ikipita hukumu yake itaongezeka na kuwa miaka 15.