Bongo5 Makala

Polisi waupata waraka wa White Widow unaodai anawalea wanae wanne kuja kuwa magaidi

Maelezo yaliyoandikwa kwa mkono kwenye kurasa 9 na mwanamke anayetafutwa zaidi duniani, Samantha Lewthwaite aka ‘White widow’ yameonesha jinsi alivyonuia kupandikiza mzuka wa kigaidi kwa wanae.

article-2444552-1884102300000578-392_634x427
Magaidi wa baadaye? Samantha Lewthwaite aliandika kuwa anawaandaa wanae, (pichani) kuja kuwa magaidi kama baba yao

Karatasi hizo, zilipatikana kwenye nyumba aliyokuwa akiishi nchini Kenya ambapo yeye na wanakarakati wengine wa kiislamu walikuwa wamepanga kushambulia hoteli mbili na kituo kikubwa cha manunuzi,.

TERROR SUSPECT, SAMANTHA LEWTHWAITE BACKGROUND-PICTURE BY MARK RICHARDS
Nyumba ya Kenya ambayo Samantha anadaiwa alikuwa akiishi

TERROR SUSPECT, SAMANTHA LEWTHWAITE BACKGROUND-PICTURE BY MARK RICHARDS

article-2444552-1884976300000578-496_634x180

Polisi pia waligundua risasi za AK-47 na picha za watoto wanne wa mwanamke huyo. Karatasi hizo zimeonesha kuwa anakuza watoto hao wafuate nyayo za baba yao, Germaine Lindsay aliyejitoa mhanga na kuua watu jijini London.

article-2444552-1884975400000578-929_634x814
Watoto wake wadogo, Abdur-Rahman mwenye miaka mitano na Surajah, 3, ni watoto wa gaidi aliyezaliwa London, Habib Saleh Ghani. Lewthwaite anatuhumiwa kupanga mashambulio kwenye maeneo ya Kenya yenye watalii wengi.

article-2444552-1884976300000578-571_306x423

Mwanamke huyo aliyebadilisha dini na kuwa muislamu, anakisiwa pia kuhusika kwenye shambulio la mwezi uliopita kwenye jengo la Westgate jijini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa. Watoto wake aliozaa na Lindsay, Abdullah, 9 na Ruqayyah, 8, wana majina ya kati Shaheed na Shahidah.

Mombasa

Lewthwaite alikuwa na ujauzito Ruqayyah kipindi Lindsay alipojilipua. Inadaiwa kuwa alikuwa amejificha nchini Tanzania au Somalia. Kwenye maelezo hayo, mwanamke huyo anaeleza jinsi alivyobarikiwa kuwa na mwanaume mgambo na jinsi alivyojitolea kuyaacha maisha ya raha kupigana na wasio waislamu.

article-2444552-1884978B00000578-222_634x720

Source: DAILY MAIL

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents