Uncategorized

Tetesi za soka barani Ulaya Jumanne hii, Bale, Fernandinho, Trippier

Real Madrid wanaangalia uwezekano wa kumuuza mshambuliaji wa kimataifa kutoka Wales, Gareth Bale msimu ujao – au wamtoe mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29- kwa mkopo ikiwa hawatampata mnunuzi anayefaa. (Marca)

Bale anaweza kujiunga na Manchester United kwa mkataba wa deni mdogo ambapo anaweza kulipwa £5m. (Marca, via Miror)

Tottenham wamejiandaa kumuuza mchezaji wa safu ya nyuma wa timu ya England Kieran Trippier
Image captionTottenham wamejiandaa kumuuza mchezaji wa safu ya nyuma wa timu ya England Kieran Trippier

Manchester City wako tayari kuvunja rekodi ya uhamisho ya £60m ili wasaini mkataba na Rodri, ambaye yuko katika kiwango cha juuzaidi cha soka. Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Uhispania mwenye umri wa miaka 22- kutoka timu ya from Atletico Madrid kama mchezaji wa kiungo cha kati anayeweza kujaza nafasi ya Mbrazili Fernandinho, mwenye umri wa miaka 33. (Telegraph)

Juventus wako tayari kuichagiza Tottenham msimu ujao kwa kumchukua Ryan Sessegnon mwenye umri wa miaka 18 anayechezewa Fulham’ safu ya nyuma kushoto. (Express)

Unai Emery atasaini mkataba na Arsenal msimu huu
Image captionUnai Emery atasaini mkataba na Arsenal msimu huu

Tottenham wamejiandaa kumuuza mchezaji wa safu ya nyuma wa timu ya England Kieran Trippier msimu ujao, huku Manchester United na Napoli wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka b28. (Sun)

Unai Emery atasaini mkataba na Arsenal msimu huu – huku mlinzi wa kimataifa Mjerumani Shkodran Mustafi, mwenye umri wa miaka 27, akiwa miongoni mwa wachezaji wanaouzwa . (mail)

Barcelona wanatarajia kumtoa mchezaji wa safu ya kati wa kimataifa wa kutoka Chile Arturo Vidal, mwenye umri wa miaka 31, kwa kurefusha mkataba wake wa sasa , utakaokamilika 2021. (Sport)

Mchezaji wa zamani wa Manchester City safu ya kati Yaya Toure, mwenye umri wa miaka 35, yuko tayari kuhamia katika Ligi kuu za soka nchini Marekani au kujiunga na timu ya Asia
Image captionMchezaji wa zamani wa Manchester City safu ya kati Yaya Toure, mwenye umri wa miaka 35, yuko tayari kuhamia katika Ligi kuu za soka nchini Marekani au kujiunga na timu ya Asia

Wolves na Sporting Lisbon ya ureno wanataka kusaini mkataba unaoweza kubadilika na mchezaji wa Liverpool Rafael Camacho mwenye umri w amiaka 19. (Birmingham Mail)

Manchester United wametoa ombi la €60m (£51.9m) kwa Bayern Munich wakiomba wasaini mkataba na Niklas Sule, mwenye umri wa miaka 23 kwa msimu unaokuja . (Sport 1, via Teamtalk)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents