Burudani
THT yatimiza Big 5
Usiku wa jana uliona kituo cha watoto wenye vipaji cha Tanzania House of Talent kikitimiza miaka mitano tangu kuanza shughuli zake za kukuza vipaji vya watoto, wengi wakiwa yatima ili kuwapa nafasi ya kujiajiri na kujikimu katika jamii.
Shughuli hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani city jijini Dar es salaam kilishereheshwa na mgeni rasmi Waziri wa habari utamaduni na michezo pamoja na aliyekuwa waziri mkuu Mhh. Edward Lowassa na mke wake Mama Regina Lowassa.
Wasanii amabao ni matunda ya THT kama Mwasiti, Lina, Barnaba na Pipi walikuwemo kutoa burudani huku wakisindikizwa na Banana Zorro aliyekuwepo kuwapiga tafu wasanii hao.
Bongo5 inawatakia Happy 5 THT na Big up kwa kazi nzuri ya kukuza vipaji vya watoto wetu wa Kitanzania.