Diamond, Davido na Yemi Alade kutumbuiza jukwaa moja na Ne-Yo kwenye tuzo za 2015 MTV MAMA
Zikiwa zimebaki siku chache kabla tuzo za MTV Africa Music Awards Kwazulu-Natal-2015 (MAMA) kutolewa, orodha ya wasanii watakaolishambulia jukwaa na kutoa burudani inazidi kuongezeka.
Baada ya msanii wa kimataifa Ne-Yo kutoka Marekani kutangazwa kuwepo, majina ya wasanii wa Afrika watakaotumbuiza yametangazwa.
Kama ilivyokuwa mwaka jana, Diamond Platnumz na Davido wametajwa kutumbuiza kwa mara nyingine kwenye tuzo za mwaka huu.
Wasanii wengine watakaotoa burudani siku hiyo ni Yemi Alade (Nigeria), Cassper Nyovest (South Africa) na Bucie (South Africa).
Announcing – #MAMAPerformers: @iam_Davido, @BUCIENQWILISO, @diamondplatnumz, @CassperNyovest & @yemialadee BOOM!! pic.twitter.com/geBkDqE92r
— MTV Base Africa (@MTVbaseAfrica) July 1, 2015
Tuzo za MAMA zitatolewa July 18, Durban, Afrika Kusini.