Habari

Kesi ya nyaraka za kodi za Trump kuanza kusikilizwa, maamuzi kutolewa kabla ya uchaguzi Marekani

Mahakama ya juu nchini Marekani Jumanne hii inaanza kusikiliza kesi kubwa ya kisiasa dhidi ya rais Donald Trump kukataa kuwasilisha nyaraka za ulipaji kodi na rekodi za kifedha kwa bunge na mwendesha mashitaka wa New York, kesi ambayo inaweza kuamua ukomo wa kinga ya urais.

Supreme Court to hear clash over Trump tax, bank records - ABC News

Majaji tisa wa mahakama ya juu ambao wapo nyumbani kwa sababu ya janga la corona, watawahoji mawakili wa pande mbili kwa njia ya simu na kurushwa moja kwa moja kupitia televisheni.

Hukumu hiyo ya mahakama ambayo inatarajiwa kabla ya mwisho wa mwezi wa sita, itawaruhusu majaji kutoa maamuzi kabla ya uchaguzi wa mwezi Novemba ambapo Trump anatafuta muhula wa pili madarakani.

Trump anakuwa rais wa kwanza tangu Richard Nixon katika miaka ya 70 kukataa kutoa nyaraka zake za ulipaji kodi na hivyo kuibua uvumi juu ya thamani halisi ya utajiri wake na uwezo wake wa kifedha.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents