Michezo
Simba SC yashindwa kutamba mbele ya URA
Klabu ya soka ya Simba imeyaaga mashindano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa URA.
Simba ambayo ilikuwa ikishika nafasi ya tatu ya kundi A kwa kuwa na jumla ya pointi nne, ilihitaji ushindi ili kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Kwa ushindi huo wa 1-0 unaifanya timu ya URA kuungana na Azam FC kutoka katika kundi hilo na kutinga hatua ya nusu fainali.